Aminiata Toure ,Ambaye
ni waziri wa Haki nchini Senegal, amependekeza makahaba wote nchini humo wapewe
vitambulisho maalum.Alisema wakati nchi hiyo ikijiandaa kwa kongamano muhimu
wiki ijayo kuhusu sheria za ukahaba.
Toure alisisitiza kuwa kadi hizo zipewe tu wanadada
waliozidi miaka 18, na watakaokiuka hilo wakamatwe na kushtakiwa.Vitambulisho
vimekuwa vikitolewa bila malipo kwa makahaba tangu miaka 20 iliyopita lakini
kwa machangudoa wanaoendesha biashara yao mjini Dakar na mitaa viungani.Waliopewa
kadi hizo walichunguzwa vikali na walihitaji kila mwezi kupita kipimo cha
HIV/Ukimwi ama maambukizi mengine ya zinaa.Waliokuwa wanaishi bila maradhi walitakiwa kutoa damu iliyowekwa
katika hifadhi na kupewa hospitali.
Waliopatikana na maambukizi madogo walitibiwa na kuruhusiwa
kwenda, na waliopatikana kuwa na vijidudu vya maambukizi walitengwa kando.Juhudi
hizo za tangu miaka ya mapema ya themanini kuhamasisha umma kuhusu janga la
ukimwi, zinaaminika kupelekea Senegal kuwa miongoni mwa mataifa yaliyo na
kiwango cha chini sana cha maambukizi ya HIV barani Afrika.
Lakini kongamano hilo la Jumatano linanuia kung’oa watoto
katika biashara hiyo na kuweka msingi wa sheria zenye uhalisi, kali na thabiti
na mikakati ya kudhibiti ukahaba nchini Senegal.Waziri huyo pia alipendekeza kikosi maalum kilichoundwa
kuwafuatilia mahakaba kipewe vifaa vya kutosha na vizuri vya kuwawezesha
kutekeleza jukumu hilo.
ALISEMA waziri huyo, “kudhibiti vyema ukahaba nchini
Senegal, twahitaji ushirikiano wa wadau kadha kama viongozi wa kidini na muhimu
zaidi wadau katika sekta ya utalii na burudani.”